Kanuni za Baraza la Sanaa la Taifa
 
 
TANGAZO LA SERIKALI NA. 322 la
tarehe 21/10/2005
SHERIA YA BARAZA LA SANAA LA TAIFA, 1984
[NA. 23 YA 1984]
|  | 
KANUNI
|  | 
Zimetungwa chini ya Kifungu cha 5
|  | 
KANUNI ZA BARAZA LA SANAA LA TAIFA,
2005
- Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Baraza la Sanaa la Taifa, 2005, na zitaanza kutumika mara baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali.
- Kwa
     madhumuni ya kanuni h izi na isipokuwa kama maelezo yatahitaji tafsiri nyingine; izi na isipokuwa kama maelezo yatahitaji tafsiri nyingine;
“Baraza” maana yake ni Baraza la Sanaa la Taifa
lililoundwa chini ya kifungu cha 3 cha Sheria ya Baraza la Sanaa la Taifa ya
mwaka 1984.
“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya
kushughulikia Sanaa
“Kamati” maana yake ni Kamati ya Sanaa ya Mkoa au
ya Wilaya
“Msajili” maana yake ni Msajili au Msajili
Msaidizi wa Vikundi, Vyama au Asasi zinazojishughulisha na sanaa
- Kutakuwepo na Baraza la Sanaa la Taifa chini ya Baraza hilo kutaunda Kamati za Sanaa za Mikoa na za Wilaya zitakazofanya kazi za Baraza katika ngazi za Mikoa na Wilaya.
- katika kila ngazi, Kamati za Sanaa zitakuwa na majukumu yafuatayo:
(a)    kubeba dhamana ya kufufua na kukuza
maendeleo na kuongeza utengenezaji wa bidhaa za sanaa ktika Mkoa au Wilaya,
ikiwa ni pamoja na kufanya utafiti wa vyombo vya muziki, nyimbo, mashairi, na
ngoma za asili na mapokeo kwa lengo la kuibua na kuendeleza utamaduni wa
Tanzania;
(b)   Kufanya utafiti wa maendeleo na uzalishaji
wa kazi za sanaa, ikiwa ni pamoja na kufanya utafiti wa viwango na thamani ya
kazi za sanaa zinazofanywa katika Mikoa au Wilaya;
(c)    Kutoa huduma za ushauri na misaada ya
kiufundi ambayo ni ya lazima au ya nyongeza katika kuendeleza shughuli za sanaa
kwa asasi na watu mbalimbali wanaojishughulisha na kazi hizi;
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
(d)   Kuandaa mipango na kuratibu shughuli za
sanaa zinazofanywa na watu au asasi mbalimbali
(e)    Kulishauri Baraza juu ya mambo yahusuyo
maendeleo na ukuzaji wa kazi za sanaa katika Mikoa au Wilaya na tTaifa kwa
ujumla;
(f)    Kutoa na kuimarisha njia za vifaa vya
mafunzo kwa ajili ya watu wanaojishughulisha, walioajiriwa na watakaoajiriwa
katika vyombo vya kazi za usanii;
(g)   Kushughulikia na kuzisaidia asasi au mtu
yeyote katika uingizaji na ununuzi wa bidhaa za sanaa kutoaka nchi za nje,
pamoja na uuzaji wa kazi za sanaa nje ya nchi
(h)   Kuhimiza maendeleo ya kazi za sanaa kwa
kuandaa na kufanya au kusimamia maonyesho, ngoma, kuendesha warsha, semina na
mashindano baina ya wasanii mbalimbali
(i)     Kufanya jingine lolote ama kwa maelekezo
ya Baraza au kwa faida ya maendeleo ya sanaa katika Wilaya, Mkoa na Taifa kwa
jumla
- Zitaundwa kamati katika Baraza, na kamati ndogo katika Kamati za Sanaa za Mikoa na za Wilaya ili kurahisisha utekelezaji wa kazi za Baraza kwa ujumla wake. Kamati hizo ni:
- Kamati ya Utendaji ya Baraza ambayo itaundwa na Wajumbe wafuatao;
(a)   
Mwenyekiti wa Baraza ambaye atakuwa Mwenyekiti wa
Kamati;
(b)  
Katibu Mtendaji wa Baraza ambaye atakuwa Katibu wa
Kamati;
(c)   
Makamu Mwenyekiti ambaye atachaguliwa na Wajumbe kutoka
miongoni mwao;
(d)  
Wajumbe wane (4) watakaochaguliwa na Baraza kutoka
miongoni mwa Wajumbe wa Baraza;
(e)   
Mhasibu wa Baraza (Hapigi Kura)
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
- Kamati ya Utendaji itakuwa na majukumu yafuatayo:
(a)    Kutekeleza maazimio na shughuli zote za
Baraza;
(b)   Kusimamia utekelezaji wa Sera ya
Utamaduni;
(c)    Kupanga tarehe za mikutano ya Baraza;
(d)   Kuandaa na kuendesha Semina na Warsha kwa
wasanii, viongozi wa vikundi, asasi au watu binafsi wanaojishughulisha na kazi
za sanaa;
(e)    Kuandaa orodha na kuweka kumbukumbu za
wasanii mahiri wa fani mbalimbali za Sanaa;
(f)    Kushughulikia mambo mengine yote yenye
manufaa kwa Baraza na maendeleo ya Sanaa kwa jumla
- Kamati ya Utafiti na Ufundi ya Baraza, au Kamati Ndogo ya Kamati ya Sanaa itakuwa na wajumbe wafuatao:
(a)    Wajumbe wasiozidi wanane (8) wenye
utaalamu wa fani mbalimbali za sanaa watakaochaguliwa na Baraza au Kamati
kutoka miongoni mwa Wajumbe wa Baraza au Kamati;
(b)   Ofisa wa Baraza au Katibu wa Kamati ya
Sanaa atakuwa Katibu wa Kamati hii
- Kamati ya Utafiti na Ufundi itakuwa na majukumu yafuatayo:
(a)    Kuchambua na kuweka takwimu thabiti ya
mahitaji ya kuendeleza sanaa mbalimbali;
(b)  
Kuratibu kazi za utafiti wa sanaa;
(c)   
Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Kamati ya Utendaji
kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo ya sanaa;
(d)  
Kuainisha sheria na kanuni za mashindano mbalimbali
(e)   
Kutengeneza programu ya Maendeleo ya Sanaa
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
- Kamati ya Fedha, Mipango na Masoko ya Baraza, au Kamati Ndogo ya Kamati ya Sanaa itakuwa na Wajumbe wafuatao:
(a)    Makamu Mwenyekiti wa Baraza au kamati
atakuwa ndiye Mwenyekiti
(b)   Mhasibu au Mweka Hazina wa Baraza au
kamati atakuwa Katibu
(c)    Wajumbe wengine watatu (3)
watakaochaguliwa kutoka miongoni mwa wajumbe wa Baraza au Kamati.
- Kamati ya Fedha, Mipango na Masoko itakuwa na majukumu yafuatayo:
(a)    Kubuni njia nzuri ya kuliingizia mapato
Baraza
(b)   Kuchambua taarifa za mapato na matumzi ya
fedha
(c)    Kusimamia miradi ya Baraza au Kamati
(d)   Kubuni mbinu za kupata masoko ya kazi za
sanaa
(e)   
Kufanya mengineyote kwa maelekezo ya Kamati ya Utendaji
- – (1) Kutakuwa na kamati fya Sanaa ya Mkoa kwa kila Mkoa ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao:
(a)   
Mwenyekiti atakuwa ni katibu Tawala wa Mkoa
(b)  
Katibu wa Kamati atakuwa Ofisa Utamaduni wa Wilaya
ambayo ni makao makuu ya Mkoa;
(c)   
Maofisa Utamaduni wa Wilaya zote zinazounda Mkoa
watakuwa ni wajumbe
(d)  
Wajumbe wengine wasiozidi watatu (3) watakaoteuliwa na
Mkuu wa Mkoa kwa kadri watakavyona inafaa
(e)   
Mweka Hazina atakayechaguliwa na wajumbe kutoka
miongoni mwao
(f)    Mjumbe mmoja mmoja kutoka kila chama cha
Sanaa cha Mkoa
  (2)
Wajumbe wote waliotajwa katika kanuni ya 12 watateuliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa
  (3) Mkuu
wa Mkoa anaweza kuteua mjumbe kujaza nafasi iliyoachwa wazi kutoakana na mjumbe
kujiuzulu, kuachishwa, kufariki, kufukuzwa au sababu nyingine.
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
  (4)
Wajumbe watakuwa madarakani kwa muda wa miaka mitatu (3) na wanaweza kuteuliwa
tena.
- –(1) Kutakuwa na kamati ya Sanaa ya Wilaya kwa kila wilaya ambayo itakuwa na Wajumbe wafuatao:-
(a)    Mwenyekiti atakuwa Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya/Mji au Manispaa;
(b)   Katibu wa Kamati atakuwa Afisa Utamaduni
wa Wilaya, Mji au Manispaa;
(c)    Wajumbe wengine watatu (3) watakaoteuliwa
na Mkuu wa Wilaya kwa kadri atakavyoona inafaa
(d)   Mweka Hazina atakayechaguliwa na Wajumbe
kutoka miongoni mwao
(e)    Mjumbe mmoja mmoja kutoka kila Chama cha
Sanaa cha Wilaya
  (2)
Wajumbe wote waliotajwa katika, Kanuni 13 watateuliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya.
  (3) Mkuu
wa Wilaya anaweza kuteua Mjumbe kujaza nafasi iliyoachwa wazi kutokana na
Mjumbe kujiuzulu, kuachishwa, kufariki, kufukuzwa au sababu nyingine.
  (4)
Wajumbe watakuwa madarakani kwa muda wa miaka mitatu (3) na wanaweza kuteuliwa
tena.
- Kutakuwa na kamati Ndogo ya Utendaji kwa kila Kamati ya Sanaa ya Mkoa au Wilaya itakayokuwa na wajumbe wafuatao:
(a)    Mwenyekiti wa Kamati ya Sanaa atakuwa
Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji
(b)   Katibu wa Kamati ya Sanaa atakuwa Katibu
wa Kamati ya Utendaji
(c)   
Makamu Mwenyekiti wa Kamati
(d)  
Mwenyekiti wa Kamati ya Utafiti na Ufundi
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
(e)   
Mwendyekiti wa Kamati ya FEdha, Mipango na Masoko
(f)   
Wajumbe wengine watatu (3) watakaochaguliwa na Kamati
ya Sanaa kutoka miongoni mwa Wajumbe wake.
(g)  
Mweka Hazina wa Kamati
- –(1) Kamati ya Sanaa ya Mkoa au ya Wilaya itafanya Mkutano wake mara moja kwa mwaka au wakati wowote kwa kikao cha dharura.
(2) Kamati ya
Utendaji ya Baraza, na Kamati Ndogo ya Utendaji ya Kamati yaSanaa itakutana
angalau mara moja kwa kila miezi miwili.
(3) Kamati
nyingine zote za Baraza, na Kamati Ndogo nyingine zote za Kamati za Mikoa na
Wilaya zilizotajwa katika Kanuni ya 5 zitafanya vikao vyake kwa maelekezo ya
Kamati ya Utendaji au kulingana na mahitaji, lakini si chini ya mara moja kwa
miezi mitatu.
- -(1) Vikao vyote vya Baraza na Kamati, kwa mujibu wa Kanuni hizi,, vitafanyika endapo idadi ya wajumbe wote waliohudhuria haipungui nusu ya idadi ya wajumbe wote wanaohusika;
(2) Endapo
Mwenyekiti aliyechaguliwa au kuteuliwa hayupo wakati wa kikao, Makamu
Mwenyekiti ataongoza kikao. Endapo Makamu Mwenyekiti naye hayupo, Wajumbe
watamchagua Mwendyekiti wa muda kuongoza kikao.
(3) Upigaji Kura
utakuwa wa siri
(4) Mwenyekiti
wa Baraza, Kamati au Kamati Ndogo atapiga kura ya uamuzi endapo kura
zililingana.
- –(1) Kutakuwepo na Msajili wa vikundi na vyama vya sanaa takayeteuliwa na Waziri
(2) kazi ya
Msajili itakuwa ni kusajili vyama, jumuia na asasi za watu binafsi
zinazojishughulisha na kazi za Sanaa.
(3) Msajili
atatekeleza majukumu yake kwa kusaidiwa na Wasajili Wasaidizi ambao ni Maofisa
Utamaduni wa Wilaya.
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
- –(1) Jumuiya, chama au asasi inayotaka kujishughulisha na kazi za sanaa itatakiwa iwe imesajiliwa.
(2) Hakuna chama au asasi itakayoruhusiwa
kuendesha shughuli za sanaa bila kusajiliwa
- –(1) Jumuiya au mtu yeyote atakayetaka kusajili asasi yake ya kushughulika na kazi za sanaa atapeleka maombi yake kwa Msajili.
Msaidizi aliyeko katika Wilaya ambayo ni makao
Makuu ya chama au asasi hiyo, Maombi hayo yaambatanishwe na:
(a)    Mhutasari wa kikao cha wanachama
kilichopitisha uamuzi wa kuandaa Chama hicho au kikundi hicho, au uthibitisho
wowote wa kuonyesha uhalali wa kumiliki asasi inayojishughulisha na kazi za
sanaa;
(b)   Nakala tatu za katiba ya chama au mwongozo
wa kikundi au asasi
(c)    Taarifa nyingineyoyote kama
itakavyoelekezwa na Msajili Msaidizi au Msajili.
(2) Baada ya Msajili Msaidizi kupokea maombi hayo,
atatoa fomu maalumu kwa mwombaji ambaye atazijaza na kasha kuzirejesha kwa
Msajili Msaidizi. Baada ya hatua hiyo, Msajili Msaidizi atatuma nyaraka zote za
maombi hayo kwa Msajili
(3) Msajili akishapokea maombi ya usajili,
atawajulisha wahusika kuhusu ama kukubaliwa au kukataliwa maombi yao katika
kipindi kisichozidi siku 14 kuanzia tarehe ya kupokeelewa maombi hayo.
- -(1) Msajili anaweza kukataa maombi yoote ya usajili ikiwa:
(a)    Jina la chama au kikundi kinachoomba
kusajiliwa linafanana na jina la Jumuiya nyingine iliyosajiliwa na Msajili wa
Sanaa au mamlaka nyingine yoyote
(b)   Kazi za chama kinachooomba kusajiliwa
zinakiuka sheria za nchi ama zinaweza kuathiri utekelezaji wa Sera za Serikali;
(c)    Anaona kuwa malengo ya Chama kinachoomba
kusajiliwa yanaweza kuhatarisha usalama na kuvuruga amani miongoni mwa jamii
kwa  ujumla na hivyo kuathiri maendeleo
ya kazi za sanaa;
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
(d)  
Kwa maelekezo ya Waziri
(2) Kila katiba
au mwongozo wowote wa chama, kikundi au mtu binafsi     
     unatakiwa kuweka wazi mambo muhimu
yafuatayo:
(a)   
Jina la chama
(b)  
Wamiliki wa chama au asasi
(c)   
Anuani kamili, ikiwa ni pamoja na mahali, sanduku la
posta, namba ya simu na kadhalika
(d)  
Madhumuni ya Chama au asasi
(e)   
Utaratibu wa uendeshaji wa shughuli za chama na kazi za
sanaa kwa ujumla wake
(3) Chama au
kikundi chochote kitakachofanya marekebisho ya kifungu chochote cha katiba
au  mwongozo wake, kitatakiwa kupata
idhini kwa Msajili kabla ya kifungu hicho kuanza kutumiwa.
- –(1) Endapo Msajili atakataa maombo yoyote ya usajili au ya kubadilisha kifungu chochote cha katiba, mwombaji anaweza kukata rufaa kwa Waziri dhidi ya uamuzi wa Msajili katika kipindi kisichozidi siku 21 tangu maombi yakataliwe.
(2) Uamuzi wa
Waziri ni wa mwisho
- –(1) Kila chama kitatakiwa kuwasilisha kwa Msajili taarifa ya utekelezaji wa shughuli zake za mwaka mzima kati ya tarehe 1 na 30 ya mwezi Juni ya kila mwaka.
(2) Kila chama
kitatakiwa kuwasilisha kwa Msajili taarifa ya mapato na matumizi ya mwaka ya
fedha zake kati ya tarehe 1-30 ya Juni ya kila mwaka
- –(1) Msajili, kwa sababu maalumu au kwa kadri atakavyoona inafaa, anaweza kukitaka chama kuwasilisha kwake taarifa yoyte inayohitajika kwa kutoa taarifa isiyopungua siku 30.
(2) Msajili,
anaweza kuamuru kiongozi yeyote wa chama kufika ofisini kwake ili kutoa taarifa
inayojitajika au kupokea maelekezo kwa kadri atakavyoona inafaa, ili mradi wito
huo uwe umetolewa si chini ya siku saba kabla ya tarehe ya kutwa.
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
(3) Msajili anaweza akatembelea eneo lolote na kwa
wakati wowote kuona utekelezaji wa kazi za sanaa baada ya kutoa taarifa kwa
chama kinachohusika
- –(1) Wakati wowote, Msajili anaweza akafuta usajili wa asasi, kikundi au chama chochote kinachoshughulikia sanaa endapo atabaini kuwa:
(a)    Chama, asasi au kikundi hicho kinachochea
uhasama miongoni mwa jamii kwa kutumia tofauti za kisiasa au udini au ubaguzi
wa aina yoyote ile;
(b)   Chama, asasi au kikundi hicho kinatekeleza
malengo tofauti nay ale yaliyoidhinishwa katika katiba yake
(c)    Chama, asasi au kikundi hicho kiantumika
na kinaelekea kutumika kuvuruga amani na misingi ya utawala bora miongoni mwa
jamii;
(d)   Chama, asasi au kikundi hicho kinavunja
sheria na kukiuka kanuni zinazoongoza kazi za sanaa nchini
(2) kabla ya kufuta usajili wa chama, asasi au
kikundi chohcote kutokana na sababu zilizotajwa katika kifungu 24 (1), Msajili
atatoa taarifa ya kusudio la kufuta usajili na kutoa fursa kwa chama, asasi au
kikundi kinachohusika kutoa sababu, katika muda usiozidi miezi mitatu, kwa ini
kisifutiwe usajili.
(3) Endapo chama kinachohusika hakitaridhishwa na
kusudio hilo la Msajili, chama hicho kinaweza kukata rufaa kwa Waziri dhini ya
kusudio la Msajili katika kipindi kisichozidi siku 21 tangu tarehe ya kupewa
taarifa. Uamuzi wa Waziri utakuwa wa mwisho.
- –(1) usajili wa vyama vya sanaa vya Wilaya, Mikoa na Taifa utazingatia aina za sanaa katika kila ngazi.
(2) Ili chama cha sanaa cha Taifa au Mkoa au Wilaya kiweze
kusajiliwa, kitatakiwa kuwe na muundo uliowekwa bayana katika katiba yake na
uliokubaliwa na wanacama wake wote au katika ngazi zake zote.
(3)  Mawakala, wakuzaji na wafanyabiashara za
sanaa watalipa ada katika ngazi huzika ili kupata idhini ya kuendesha
shughulizao.
(4) Mawakala,
wakuzaji na wafanyabiashara za sanaa, watatakiwa kuwa na mikataba na wasanii
inayotambuliwa na Baraza
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
(5) Watumiaji wa kazi za sanaa kwa lengo la
kufundishia au kutoa mihadhara wanatakiwa kuomba na kuapta ridhaa ya
kimaandishi ya mbunifu wa sanaa husika.
(6) Nakala za mikataba au vibali zitahifadhiwa na
Baraza au Kamati inayosusika.
- –(1) Maonyesho, mashindano na matamasha ya sanaa yatafanyika baada ya kupata kibali katika kila ngazi kwa utaratibu ufuatao:
(a)    Kwa maonyesho, mashindano na matamasha ya
sanaa nayayoshirikisha zaidi ya mkoa mmoja, kibali kitaombwa kutoka kwa Baraza
la Sanaa la Taifa
(b)   Kwa maonyesho., mashindano ya matamasha ya
sanaa yanayoshirikisha zaidi ya wilaya moja kati ya wilaya za mkoa husika au
wilaya isiyo ya mkoa huo, kibali kitaombwa kutoka kwa Kamati ya Sanaa ya Mkoa
huo.
(c)    Kwa maonyesho, mashindano na matamasha ya
sanaa yanayoshirikisha wilaya moja, kibali kitaombwa kutoaka Kamati ya Sanaa
yinayohusika;
(2) Vibali vyote vitatolewa kwa kuzingatia masharti
yafuatayo.
     
(a)  Shughuli za sanaa
zilizoombewa na kupatiwa kibali zitafanyika kwa 
            kufuata
sheria, kanuni na taratibu zilizopo;
     (b) Shughuli za sanaa zilizoombewa na
kupatiwa kibali zifanyike bila 
           kuwadhalilisha wasanii au dhadhira au kufanya jambo lolote linalokiuka 
          
maadili na utamaduni wa Mtanzania
     (c)
Shughuli hizo zilenge katika kuelimisha, kukosoa, kuburudisha na 
         
kuhamasisha umma katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii;
(d)   Maombi ya vibali vya maonyesho
yawasilishwe kenye ngazi inayohusika si chini ya siku kumi na nne kabla ya siku
ya maonyesho
(3) Waandaaji wa
maonyesho wazingatie yafuatayo:
     (a) Watoto chini ya umri wa miaka 18
hawataruhusiwa kuingia katika kumbi 
          au sehemu zinazouzwa pombe wakati wa
maonyesho ya sanaa;
    (b) Mavazi na maleba ya wasanii hayana budi
kuwa ya heshima;
    (c) 
Sanaa zinazolengwa kwa watu wazima zisionyeshwe kwa watoto
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
    (d)
Watoto wasiruhusiwe kuwepo katika kumbi au maeneo ya maonyesho 
         
baada ya saa 2.00 usiku
(4) Maonyesho yanaweza kusimamishwa iwapo
itabainika kuwa yanakiuka taratibu, kanuni au sheria zilizowekwa, au hayazingatii
masharti ya kibali.  
- –(1) Kumbi zote za maonyesho ya sanaa zitapangwa kwa madaraja kwa utaratibu ufuatao:
(a)   
Daraja A – Kumbi ambazo sauti haisikiki nje
(b)  
Daraja B – Maeneo ya wazi ambayo ni maalumu kwa
maonyesho ya sanaa
(c)   
Daraja C – Kumbi zisizozuia sauti kutoka nje ambazo
zimejengwa kwenye makazi ya watu au karibu na hospitali, shule, misikiti,
makanisa n.k.
(2) Kumbi
zitatumika kwa shughuli za maonyesho ya sanaa kwa utaratibu ufuatao:
      (a) 
Kumbi za daraja A zinaweza kutumika kwa shughuli za maonyesho ya 
            sanaa wakati wowote kwa kuzingatia
masharti ya mamlaka zilizotoa vibali 
            vya maonyesho hayo;
     (b) 
Kumbi za daraja B zinaweza kuendesha shughuli za maonyesho ya sanaa 
           kuanzia saa 10.00 jioni na si zaidi
ya saa 5 usiku kwa siku za kuanzia 
           Jumatatu hadi Ijumaa. Siku za
Jumamosi, Jumapili na sikukuu, maonyesho 
           yanaweza kuanza mapema na kumalizika
si zaidi ya saa 7.00 usiku
(c) Kumbi za
daraja C zinaweza kuendesha shughuli za maonyesho ya sanaa 
     kuanzia saa 10.00 jioni na si zaidi ya saa
3.00 usiku kwa siku zote.
- –(1) Wasanii au vikundi vya aina yoyote ya sanaa wanaweza kwenda kufanya maonyesho ya sanaa nje ya nchi baada ya kupata kibali kutoka Baraza la Sanaa la Taifa. Aidha, vikundi vya maonyesho ya sanaa au wasanii binafsi kutoka nje ya Tanzania wanaweza kufanya maonyesho yao baada ya kupata kibali kutoka Baraza la Sanaa la Taifa na mamlaka nyinginezo zinazohusika na uingiaji wa wageni nchini.
(2) vibali vya
kwenda nje ya nchi au kuruhusu wageni kufanya maonyesho yao hapa nchini vitatolewa baada ya mwombaji
kuthibitisha uwezo wake wa kumudu gharama za uendeshaji wa maonyesho hayo,
ikiwa ni pamoja na gharama za wasanii kujikimu wakiwa huko ugenini au hapa
nchini.
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
- ghughuli zote za sanaa zitafanyika kwa kuzingatia sheria ya |Hakimiliki na hakishiriki
- –(1) chama, kikundi, asasi au mtu yeyote atakayebainika kuvunja au kukiuka kifungu chochote cha Kanuni hizi anaweza kuchukuliwa hatua zifuatazo:
(a)    Kutozwa faini isiyopungua shilingi elfu
hamsini (Sh. 50,000/=)
(b)  
Kufuatiwa usajili
(c)   
Kusimamishwa kuendesha hughuli za sanaa
(d)  
Kuzuiwa kujishughulisha na kazi za sanaa kwa kipindi
kisichopungua miezi sita
(e)   
Kuzuiwa kujishughulisha na kazi za sanaa maisha, kwa
kubainika kujihusisha na vitendo vya kupokea au kutoa rushwa.
(2) Adhabu
zilizotajwa katika Kanuni ya 31 (1) zinaweza kutolewa mojamoja au kwa pamoja
julingana na uzito wa kosa.
- Kutakuwepo na ada mbalimbali kwa huduma zitakazotolewa kwa Baraza la Sanaa la Taifa na ngazi zake kama itakavyoonyeshwa katika jedwali iliyomo katika Kanuni hizi.
- Baraza, kwa kibali cha Waziri inaweza kurekebisha kanuni hizi kama itakavyoonekana inafaa.
Kanuni
za Baraza la Sanaa la Taifa
|  | 
Tangazo la
Serikali Na. 322 (linaendelea)
JEDWALI
|  | 
(Kifungucha 32)
ADA ZA HUDUMA
KAMA ZILIVYOREKEBISHWA NA
WRAKA WA  WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI NA
MICHEZO, YA TAREHE 16/-7/2009
(Tangazo la Serikali Na. 322 la tarehe 21/10/2005 la
Kanuni za BASATA na marekebisho yaliyofanyika kwa idhini ya Waziri wa Habari,
Utamaduni na Michezo ya tarehe 16 Julai 2009)
| 
NA | 
MHUSIKA | 
USAJILI 
Tsh. | 
KIBALI 
Tsh. | 
FAINI 
Tsh. | 
| 
1 | 
TAASISI/VYAMA | 
30,000 | 
50,000 |  | 
| 
2 | 
PROMOTA/MAKAMPUNI | 
30,000 | 
200,000 |  | 
| 
3 | 
WASANII BINAFSI | 
30,000 | 
40,000 |  | 
| 
4 | 
VIKUNDI | 
30,000 | 
40,000 |  | 
| 
5 | 
FOMU YA USAJILI | 
5,000 | 
- |  | 
| 
6 | 
VIBALI VYA KAWAIDA KUINGIA NDANI YA NCHI | 
- | 
1,000,000 |  | 
| 
7 | 
VIBALI VYA DHARURA KUINGIA NDANI YA NCHI | 
- | 
1,500,000 |  | 
| 
8 | 
VIBALI KUENDESHA MASHINDANO  
a.       MASHINDANO
  YA KIBIASHARA 
b.       MASHINDANO
  YASIYO YA KIBIASHARA | 
- 
- | 
1,500,000 
100,000 |  | 
| 
9 | 
VIBALI VYA KUENDESHA MATAMASHA: 
c.       MATAMASHA
  YA KIBIASHARA 
d.       MATAMASHA
  YASIYO YA KIBIASHARA | 
- 
- | 
1,500,000 
100,000 |  | 
| 
10 | 
WAFANYA BIASHARA NDOGONDOGO | 
30,000 | 
30,000 |  | 
| 
11 | 
KUMBI
  ZA MAONYESHO YA JUKWAANI: 
a)      
  Zenye ukubwa wa kukaa watu wasiozidi 350 
b)       Zenye
  ukubwa wa kukaa watu   351 – 550 
c)       Zenye
  ukubwa wa kukaa watu   551 – 750 
d)     Zenye ukubwa wa kukaa watu   751 na kuendelea |  | 
300,000 
500,000 
700,000 
1,000,000 |  | 
| 
12 | 
UPOTEVU WA CHETI | 
- | 
- | 
15,000 | 
| 
13 | 
KUBADILISHA JINA LILILOSAJILIWA  | 
- | 
- | 
20,000 | 
| 
14 | 
KUTANGAZA/KUENDESHA SHUGHULI ZA SANAA BILA KIBALI
  CHA BASATA | 
- | 
- | 
500,000 | 
| 
 
              
  Kibali hiki hutolewa bure. | ||||
Dar es salaam                                                                          J.J.
Mungai (Mb)
20 Julai, 2005                                                              Waziri
wa Elimu na Utamaduni
Certificate of the Permanent National Votgers Register
|  | 
GOVENMNENT NOTICE  NO 323 PUBLISHED ON 21/10/2005
THE PRESIDENTIAL
ANDPARLIAMENTARY ELECTIONS
(REGISTRATION OF
VOGERS)REGULATIONS, 2004
NOTICE
Made under regulation 31 (3)
CERTIFICATION OF THE PERMANENT NATIONAL VOTERS
REGISTER
Citation      1. This Notice shall be cited as the
certification of the Permanent 
                                  national
Voters  Register
Certification 2.-(1) The Director of
Elections hebery, certifies that, the Permanent 
Of the                     National Voters’ Register shall come into
force with effecfrom 
register                   1st   October 2005
(2) The Permanent National Voters’
Register shall replace all the Provisional Voters’ Register and shall remain in
force until another new register is prepared and certified in accordance with
the Regulations.
Made by the Director of Elections
this 1st day of October 2005
                            Dar es salaam                                              Rajabu
R. Kiravu
                           October, 2005                                           Director of elections
Certificate of the Permanent National Votgers Register
|  | 
GOVENMNENT NOTICE  NO 323 PUBLISHED ON 21/10/2005
THE COUNCILLORS’
ELECTIONS [REGISTRATION OF VOTERS] REGULATIONS, 2004
NOTICE
  Made under regulation 30 (3)
|  | 
CERTIFICATION OF THE PERMANENT NATIONAL VOTERS
REGISTER
1. This Notice shall be cited as
the certification of the Permanent National    
Citation
     voters 
Register.
2. –(1) The Director of elections
hereby, certifies that, the Permanent           
Certification
      National voters’ Register shall come into
force with effect from                       of the 
      October 2005.                                                                                       
      registration
     (2) The Permanent National Voters’
Register shall replace all 
       The Provisional Voters’ Register and
shall remain in force until 
       New register is prepared and certified
in accordance with the 
       Regulations
Made by the Director of Elections this 1st day of October
2005
Dar es salaam                                                                          Rajabu
R. Kiravu
October 2005                                                                       Director of Elections



 
No comments:
Post a Comment